Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi.

Timu ya Jeshi la Polisi itakayoshiriki michezo ya Shirikisho la Wakuu wa Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO Games) inatarajiwa kuondoka Jumanne Agosti 13 mwaka huu kuelekea katika jiji la Windhock nchini Namibia kwa ajili ya michezo hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Afisa Michezo wa Jeshi la Polisi Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Jonas Mahanga alisema timu hiyo itaondoka na wanamichezo 67 ambao wanaunda timu za Mpira wa miguu wanaume, Mpira wa pete Wanawake, Riadha wanaumwe na wanawake na mchezo wa Vishale (Dats).

Mahanga alisema timu hiyo inaendelea na mazoezi katika kambi yao ya maandalizi iliyopo katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) ambapo mpaka hivi sasa wameshacheza michezo kadhaa ya kujipima nguvu na kufanikiwa kufanya vizuri.

Alisema michezo hiyo itashirikisha Nchi kumi na nne (14) katika michezo mbalimbali na lengo la michezo hiyo ni kujenga ushirikiano wa Majeshi ya Polisi kwa nchi wanachama wa SARPCCO katika kukabiliana na uhalifu.

“Michezo hii pamoja na kuweka vyema kiafya miili ya Askari wetu, lakini pia itakuwa ni fursa kwa Askari wetu kufahamiana na wenzao na kubadilishana uzoefu katika kukabiliana na uhalifu hasa unaovuka mipaka”Alisema Mahanga.

Mara ya mwisho Tanzania kushiriki katika michezo hiyo ilikuwa mwaka 2009 nchini Malawi ambapo timu hiyo ilinyakua ushindi wa pili kiujumla .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...