Mkuu wa kituo cha polisi Mererani, Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, SP Ally Mohamed Mkalipa, akisalimiana na Abdulhalim Humudi, wakati akiikagua timu ya Simba ilipocheza juzi na timu ya Tanzanite FC, baada ya kutembelea machimbo ya madini ya Tanzanite.
Mchezaji wa timu ya soka ya Simba SC ya jijini Dar es salaam, Edward Christopher, akipatiwa huduma ya kusuguliwa kwenye saluni ya kisasa ya Nick Babershop ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, baada ya mchezo wa kirafiki uliofanyika jana na Simba ilishinda bao 1-0.Picha na Woinde Shizza,Mererani.

Na Woinde Shizza,Manyara

Timu ya soka ya Simba SC ya Jijini Dar es salaam jana imetembelea machimbo ya madini ya Tanzanite ambapo hapa duniani yanapatikana Mji mdogo wa Mirerani, Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara,Tanzania.

Wachezaji hao wakiongozwa na viongozi wao Makamu Mwenyekiti, Joseph Itangire (Mzee Kinesi) na kocha mkuu Abdalah Kibadeni, walitembelea kampuni ya TanzaniteOne na kujionea namna shughuli za uchimbaji zinavyofanyika.

Hata hivyo, wachezaji hao wakizungumza kwenye machimbo hayo ya madini ya Tanzanite, walisema hiyo ni mara yao ya kwanza kutembelea machimbo hayo kwani awali walikuwa wanasikia Tanzanite katika vyombo vya habari pekee.

Walipotembelea machimbo hayo pia walicheza mchezo wa kirafiki na timu ya Tanzanite FC inayomilikwa na Jofrey Nyigu (Mnyalu) na wakaifunga bao 1-0 lililotiwa kimiani na mshambuliaji wao hatari Abdalah Seseme.

Seseme alifunga bao hilo baada ya kupewa pasi na Ramadhan Singano “Messi” aliyewachambua mabeki wa Tanzanite FC, Elibariki Bryson na Abdilahi Yusuph walioshindwa kumpa ulinzi kipa wao Achibald Kileo.

Baada ya kumalizika mchezo huo wa kirafiki, timu ya Simba ilikwenda kwenye saluni ya kisasa ya Nick Baber shop iliyopo Mirerani na kufanyiwa huduma ya kuchuliwa misuli, kuoga, kusuguliwa uso,miguu na kunyolewa nywele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...