Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiongea na moja ya
washindi wakati Airtel ilipochezesha droo ya saba ya washindi wa
shilingi milioni moja kila siku wa promosheni ya Airtel yatosha
ambapo mpaka sasa zaidi ya shilingi million 44 zimeshatolewa.
Akishuhudia ni Msimamizi wa bodi ya michezo ya Bahati nasibu.
Washindi wa siku wa shilingi milioni moja wa promosheni ya Airtel
yatosha bwana Thomasi Joackim Chali na Abdallah Omari Muhomba kwa
pamoja wakionyesha furaha mara baada ya kukabithiwa zawadi za pesa
taslimu baada ya kuibuka washindi wa siku wa promosheni ya Airtel
yatosha.
Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel imetangaza washindi wake saba wa
wiki ya saba ya Airtel Yatosha promosheni na kukabidhi zawadi za
washindi wa wiki ya sita wa promosheni ya Airtel Yatosha.
Airtel imechezesha droo ya wiki ya saba ya promosheni ya Airtel
yatosha Jana katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco jijini Dar
es saalam ambapo wateja saba wameibuka washindi wa kitita cha
shilingi million 1 kila mmoja.
Washindi hao ni pamoja na Theresia Martine Komba wa Morogoro -Mkulima,
John Kimoro wa kondo Dodoma -Mwalimu, Yohanna Masunga Zengo wa Maswa
Shinyanga -Mkulima, Isabellah Joseph wa Chamwino Dodoma -Mwalimu,
Nassor Mohammed Nassor wa Kariakoo DSM -Mfanyabiashara, Modest
Laurian Mussa wa Bukoba Kagera -Mfanyabiashara na Masanja Mwanamenda
wa Nkyala Singida -Mfanyabiashara.
Wakati huo huo Airtel imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia
promosheni ya Airtel Yatosha ambapo washindi wa wiki ya sita nao
walikabidhiwa zawadi zao ambapo kila mmoja aliondoka na shillingi
milioni moja.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo katika ofisi za makao makuu ya
Airtel bwana Abdallah Omari Muhomba mmoja wa washindi wa million 1
alisema, "nashindwa jinsi ya kuongea lakini nawashukuru sana Airtel
kwa kuweza kunizawadia shilingi milioni 1 ambazo kwangu nikama ndoto.
Nategemea kutumia pesa hizi kujiendeleza kiuchumi na maaendeleo ya
familia yangu. Binafsi nachukua fursa hii kuwaasa watanzania kushiriki
katika promosheni hizi za Airtel na kwa hakika wataamka washindi kama
mimi hivi leo".
Kwa upande wake bwana Thomas Joachim Chali ambaye pia ni Mshindi wa
wiki ya sita alisema, "anawashukuru Airtel kwa kuanzisha promosheni
yaAirtel Yatosha , na kuahidi kuzitumia pesa zake kuendeleza na
kupanua biashara kwa kuwa hiyo ndio shughuli kubwa anayoifanya".
Akiongea wakati wa makabidhiano hayo kwa washindi hao Meneja uhusiano
wa Airtel bwana Jackson Mmbando alisema, "leo tunao washindi saba
waliojishindia shilingi milioni 1 kila moja katika droo ya wiki.
Tumeendelea kushuhudia watanzania na wateja wetu wakiibuka mamilionea
kila siku na kila mwezi kupitia promosheni hii ya Airtel Yatosha.
Tunaahidi kuendelea kuwazawadia wateja wetu huku tukiboresha huduma
zetu , na kuwapata wateja wetu huduma bora zenye gharama nafuu kupitia
huduma yetu poa ya Airtel Yatosha inayomuwezesha mteja kuwasiliana na
mitandao mengine ya simu za mkononi kwa bei poa na kupata vifurushi
vya maongezi bila kulipia gharama ya ziada". Aliongeza Mmbando.
Promosheni ya Airtel Yatosha bado inaendelea na wateja wetu wa Airtel
Yatosha bado wananafasi ya kuendelea kujishindia pesa taslim na Nyumba
mbili za kifahari zilizopo Kigamboni bado kushindaniwa.
Droo itakayomchagua mshindi wa nyumba kwa mwezi huu inatarajiwa
kuchezeshwa tarehe 5/9/2013 saa tano asubuhi. hii itachagua mshindi
mmoja kati ya wateja wote waliotumia huduma ya Airtel yatosha kwa
mwezi huu.
Ili mteja wa Airtel aweze kushiriki anatakiwa kujiunga na vifurushi
vya Airtel Yatosha kwa kupiga *149*99# na kujiunga na vivurushi vya
Airtel Yatosha. Kila unapojiunga na kifurushi unaingia moja kwa moja
kwenye droo ya kushinda.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...