Na Abdulaziz video, Kilwa
 Wakaazi  wa kijiji cha Kiranjeranje wilayani Kilwa, Mkoani Lindi,  walifunga barabara kuu ya Kibiti-Lindi-Mtwara kwa kuweka magogo, na mawe na kusababisha abiria na magari zaidi ya 50 kukaa kwa kipindi cha masaa kadhaa kabla ya kutawanywa na kikosi cha kutuliza Ghasia,FFU.
Tukio hilo limetokea baada ya mwendesha bodaboda mkazi wa kijiji hicho Bakari Magoyo (38) kugongwa na gari namba T489 AGA wakati alipokuwa anavuka barabara hiyo. 
Wakizungumza kwa niaba ya wananchi wenzao waliokuwepo baada ya kutawanywa kwenye tukio hilo,wakaazi hao walisema kuwa wameamua kufunga barabara hiyo kwa kuweka mawe na magogo ili kuishinikiza serikali kuweka matuta ya kupunguza mwendo kasi wa magari kwenye eneo la makazi ya watu na ajali zinazotokea mfululizo katika eneo hilo. 
 ,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga amewataka wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi badala yake wafuate kanuni na taratibu za kisheria.
Kamanda  Mwakajinga alieleza kusikitishwa kwake na tukio la kupigwa kwa dereva wa gari hilo, Omary Mkuwili, huku gari lake likivunjwavunjwa na kuibiwa karibu vifaa vyote baada ya ajali hiyo.
  Aidha alibainisha kuwa Mwendesha pikipiki aliegongwa alikimbizwa hospitali ya mkoa ya Sokoine kwa ajili ya matibabu zaidi huku dereva wa gari iliyogonga alipata majeraha makubwa baada ya kupata kipigo na wananchi wenye hasira kali
Gari lililopata ajali kijijini Kiranjeranje, wilayani Kilwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Nyinyi wananchi wacheni kupiga madereva bila ya kuangalia kosa ni la nani.

    Waendesha bodaboda wengi hawazingatii sheria na hujivukia tu barabara au kuendesha kwa spidi kubwa kama sheria za barabara haziwahusu.

    ReplyDelete
  2. Hilo neno "Kijijiji" lina maanisha nini? Maana siku hizi kiswahili kina kua kwa kasi.

    ReplyDelete
  3. Ohhh Majanga!

    Mdau Omari Mkuwili amenunua kiji Korola chake jijini Darisalama akasema acha niende nyumbani Kusini nikawasalimie anafika kijijini Kiranjeranje-Kilwa Wananchi wenye hasira kali wana mwangukia kwa maqkonde na magumi!

    Kwa nini wanakijiji msingoje Trafiki apime kwanza ajali?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...