Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Simbani, Bw. Ombeni Ally (katikati), akipokea vitabu toka kwa mwakilishi wa shirika la HUC Bw. Ramadhani Kuchimba, Jumatatu Septemba 23, 2013. Kulia ni Afisa Mtendaji wa Simbani, Bw. Kuboja Majogoro.
Ndivyo wasemavyo wanafunzi wa Shule ya Sekondari Simbani iliyo mkoa wa Pwani, wakifurahia vitabu vya msaada toka HUC, Jumatatu, Septemba 23, 2013. HUC ni shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake Marekani, linalosaidia upatikanaji wa maji ya kunywa safi na salama na vifaa vya elimu kwa maeneo yenye upungufu wa huduma za kijamii.
Mwakilishi wa Shirika la HUC nchini Tanzania, Bw. Ramadhan Kuchimba (kushoto), akimkabidhi vitabu Meneja wa Kibaha Children’s Village Centre, Bw. Deogratius Mosha, Jumatatu Septemba 23, 2013, Mkoani Pwani.
Wafanyakazi wa Kibaha Children’s Village Centre wakigawa vitabu vya msaada toka Shirika la HUC. Kushoto ni Mwakilishi wa HUC Tanzania, Bw. Ramadhan Kuchimba.
Meneja Mtandao usio wa Kijamii wa HUC, Bw. Nathan Mpangala (kushoto) akigawa vitabu kwa watoto wa Kibaha Children’s Village Centre, Jumatatu Septemba 23, 2013. Kituo hiko kiko Kibaha, Pwani.
Wakati wa kujisomea: Watoto wa Kibaha Children’s Village Centre wakifurahia vitabu vya msaada toka Shirika la Help for Underserved Communities Inc. (HUC), Jumatatu septemba 23, 2013.
Muda mfupi baada ya HUC kukabidhi vitabu vya msaada katika kituo cha Kibaha Children’s Village Centre.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...