Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

 TAARIFA KWA UMMA
 Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Uongozi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadau wa tasnia ya utalii nchini wanayo furaha kuwakaribisha wananchi wote na wadau mbalimbali katika maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka 2013 ambayo Kitaifa yatafanyika Mkoa wa Mwanza.
Siku ya Utalii Duniani huadhimishwa tarehe 27 Septemba ya kila mwaka ambapo kila nchi mwanachama wa Shirika la Utalii Duniani husheherekea siku hii. Kwa mwaka huu Kimataifa, maadhimisho haya yatafanyika katika Visiwa vya Maldives.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Utalii na Maji – Kulinda Hatma Yetu (Tourism and Water – Protecting Our Common Future)”. Kwa kuzingatia kauli mbiu hii, tunawajulisha wadau wote katika nyanja mbalimbali za uhifadhi mazingira, matumizi ya teknolojia sanifu, wafanyabiashara wa tasnia ya utalii na maliasili, wadau wa sekta ya maji, taasisi za elimu, wanasiasa, viongozi na wataalamu mbalimbali kushiriki katika wiki ya maadhimisho ya utalii duniani.
Shughuli zitakazofanyika ni pamoja na tafsiri ya kauli mbiu katika Nyanja mbalimbali kama, mashindano ya uandishi wa insha mbalimbali kuhusiana na mada, michezo na burudani mbalimbali, maonesho ya utalii, malikale, misitu na masuala ya uhifadhi kwa ujumla,  teknolojia mbalimbali, pamoja na ziara ya kutembelea Hifadhi ya Saanane.
Wananchi pamoja na wadau wote mnakaribishwa sana kushiriki katika maadhimisho haya.
“Kumbuka Utalii ni nyenzo ya kuhamasisha uhifadhi kwa uhai na ustawi wa Taifa”
Imetolewa na:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Maliasili na Utalii,
S.L.P 9372,
DAR ES SALAAM.

Simu: 255-22-2864230
Barua pepe: ps@mnrt.go.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...