Katibu wa Taswa Jijini Arusha,Mussa Juma akiongea na waandishi wa habari kuhusiana Tamasha la Taswa linalotarajiwa kufanyika kesho katika kiwanja cha general tyre,jijini humo.Kushoto ni Afisa wa Kinywaji cha Vita Malt ambao ni sehemu ya wadhamini wa Tamasha hilo,Deogratius Katambi.

Na Woinde Shizza,Arusha

Tamasha la michezo la waandishi wa habari za Michezo nchini (TASWA) linatarajiwa kufanyika kesho September 8 katika viwanja vya general tyre vilivyopo njiro jijini hapa.

Akiongelea tamasha hilo katibu wa chama cha waandishi wa habari za michezo mkoani wa Arusha,Musa Juma alisema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na jumla ya timu 12 zinatarajiwa kushiriki katika tamasha hilo.

Alisema kuwa michezo mbali mbali itachezwa katika tamasha hili ikiwa ni pamoja na kufukuza kuku,kukimbia na magunia,mpira wa miguu ,mpira wa pete pamoja na michezo mingine mbalimbali sambamba na burudani mbalimbali za muzikikutoka katika sehemu na bendi mbalimbali.

Alisema kuwa hili nitamasha la nane kufanyika na kwa mara hii wameboresha zaidi kwani zawadi zimeongezeka tofauti na kipindi kingine.

Amewasihi wadau mbalimbali kujitokeza katika tamasha hili kwani tamasha hili ni lakihistoria kutoka na waandishi mbalimbali kushiriki kutoka katika mikoa mbalimbali.

Alitaja baadhi ya timu zitakazo shiriki katika tamasha hili kuwa ni pamoja na timu ya taswa ya jijini dar es salaamu ambapo inatarajiwa kuwasili leo timu ya taswa arusha ambao ni wenyeji wa bonanza hili,timu ya taswa manyara ,timu ya triple a fm ,sunrise fm,radio five pamoja na timu nyingine nyingi ikiwemo timu ya tbl ambao ni wathamini wakuu pamoja na timu ya wazee klabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...