Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya akiongea kuhusu kuboreshwa kwa huduma mpya ya Airtel Yatosha inayomwenzesha mteja wa Airtel kupata kifurushi cha maongezi , sms na internet na kuwasiliana na mitandao yoyote nchini, sasa kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125MB.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza kuboresha vifurushi vyake vya huduma ya Airtel yatosha hivyo kuvifanya kuwa bora, vya ushindani na gharama nafuu nchini.

Akiongea kuhusu kuboreshwa kwa huduma hiyo , Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya alisema "huduma ya Airtel Yatosha inaendelea kutosha kuliko yoyote nchini! sasa vifurushi vya Airtel yatosha vya siku zimeendelea kuboreshwa na kuwa vya gharama nafuu zaidi, kwa shilingi 499 mteja anapata dakika 20, sms 300 pamoja na kifurushi cha internet cha 125MB. Bei ni poa na ya gharama nafuu ukilinganisha na huduma nyingine za vifurushi zinazotelewa sokoni"

Bi Singano alisema Sambamba na hili vifurushi vya Airtel yatosha vinamuwezesha mteja kupiga simu kwenda mtandao wowote ule nchini wakati wowote masaa 25 yaani mteja anafaidika na vifurushi hivi kwa masaa 24 na 1 la nyongeza siku saba za wiki.

Kikubwa na kizuri zaidi mteja anapojiunga na vifurushi hivi anapata nafasi ya kuingia kwenye promosheni yetu kabambe ya Airtel Yatosha Shinda Nyumba na kujishindia pesa taslimu au nyumba za kisasa zilizoko Kigamboni jijini Dar es saalam".

"Airtel inaendelea na dhamira yake ya kuboresha huduma zake ikiwemo Airtel money yatosha pamoja na vifurushi vya Airtel yatosha vilivyo na gharama nafuu na kukuwezesha kuwasiliana kwa gharama nafuu zaidi ndani na nje ya nchi". aliongeza mmbando.

Kujiunga na vifurushi mbalimbali vya Airtel yatosha mteja anatakiwa kupiga *149*99# na kuchagua kifurushi kinachokithi mahitaji yake. Airtel yatosha inapatikana katika vifurushi vya siku, wiki au mwezi na vifurushi vyake vinadumu kwa masaa 25 kwa siku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...