Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akizungumza na Balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Frederiks masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uholanzi. Balozi huyo alimuhakikishia Dk Nchimbi ushirikiano wa hali ya juu kati ya nchi yake na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwa Waziri Nchimbi, jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimshukuru Balozi wa Uholanzi nchini, Jaap Frederiks kwa kumtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo kwa lengo ya kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na Nchi ya Uholanzi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...