Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa
Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika Mapambano
ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA) ambaye pia ni Waziri
wa Mambo ya Ndani wa nchini Rwanda, Sheikh Mussa Fazil Harerimana wakiwa tayari
kuipokea bendera ya RECSA kabla ya Dk Nchimbi kukabidhiwa bendera hiyo ikiwa ni
ishara ya kukabidhiwa kuliongoza baraza hilo kwa kipindi cha miaka miwili.
Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya
Serena, jijini Dar es Salaam leo. Nchi wanachama wa RECSA ni Burundi, Congo,
Djibout, Ethiopia, Eritrea, Kenya, Rwanda, Sudan, Uganda na Tanzania
Mwenyekiti
mpya wa Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika
Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA) na Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na wajumbe wa Baraza
hilo pamoja na watendaji wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na
wananchi mablimbali baada ya kukabidhiwa uenyekiti huo katika hafla
iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Serena, jijini Dar es
Salaam leo. Nchi wanachama wa RECSA ni Burundi, Congo, Djibout, Ethiopia,
Eritrea, Kenya, Rwanda, Sudan, Uganda na Tanzania.
Mwenyekiti
mpya wa Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika
Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA) na Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimkabidhi zawadi
mwenyekiti aliyemaliza muda wake wa kuiongoza RECSA ambaye ni Waziri wa Mambo
ya Ndani wa nchini Rwanda, Sheikh Mussa Fazil Harerimana. Hafla ya makabidhiano
hayo iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Serena, jijini Dar es
Salaam leo. Nchi wanachama wa RECSA ni Burundi, Congo, Djibout, Ethiopia,
Eritrea, Kenya, Rwanda, Sudan, Uganda na Tanzania.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (kulia viti vya
mbele) akiwa na watendaji wengine wakuu wa wizara hiyo pamoja na wageni
waalikwa wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti mpya wa Baraza la Mawaziri wa Nchi
za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti
Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA) na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk
Emmanuel Nchimbi (hayupo pichani) mara baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa RECSA
na Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchini Rwanda, Sheikh Mussa Fazil Harerimana.
Hafla hiyo makabidhiano ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Serena,
jijini Dar es Salaam leo. Nchi wanachama wa RECSA ni Burundi, Congo, Djibout,
Ethiopia, Eritrea, Kenya, Rwanda, Sudan, Uganda na Tanzania. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...