KAMPUNI ya Ndege ya  Hainan ya China imekubali kufanya safari za ndege za moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania ili kukuza sekta ya biashara na utalii baina ya nchi hizo mbili.
 
Ahadi hiyo imetolewa leo mchana (Alhamisi, Oktoba 24, 2013) na Mwenyekiti wa Shirika la Ndege la Hainan (Hainan Airlines), Bw. Chen Feng baada ya kuombwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye katika mazungumzo yao alimwomba akubali ndege za shirika lake ziwe zinatua Tanzania. Ndege za shirika hilo zinafanya safari kati ya China na Angola kupitia anga la Tanzania.
 
Waziri Mkuu ambaye yuko ziara ya kikazi nchini hapa, moja ya eneo ambalo amekuwa anaziomba kampuni za ndege za China ni kufikiria kufanya safari ya moja kwa moja kati ya nchi hizo mbili ili kukuza biashara pamoja na utalii pamoja na kuja kuweza katika ujenzi wa hoteli za kitalii. Pia alisema kuna Watanzania wengi ambao wanakuja China kuchukua bidhaa hapa China lakini wanalazimika kuunganisha safari mara tatu hadi nne kabla hawajafika China jambo ambalo alisema linawaongezea gharama mno.
 
Akijibu maombi hayo ya Waziri Mkuu, Bw. Chen alisema kutokana na urafiki uliopo baina ya nchi hizo mbili, maombi yake watayafanyia kazi na mojawapo ni hilo la kufungua safari za moja kwa moja za ndege kutoka China kwenda Tanzania.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...