TAWALA WA MIKOA Katibu mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. George Yambesi leo amefungua rasmi mafunzo ya mfumo wa kompyuta wa kusimamia rasilimali watu Serekalini, kwa Makatibu Tawala wa mikoa (RAS) na Wakurugenzi (DED) kutoka mikoa na wilaya mbalimbali Tanzania. 
Maofisa hawa wa Serikali wamegawanywa katika makundi na watahudhuria mafunzo hayo kwa siku tatu tatu. Mafunzo hayo yanafanyika katika maabara za kompyuta za Wakala wa Serikali wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (Tanzania Global Learning Agency, TaGLA).
Katibu Mkuu Bw. Yambesi (katikati) akifungua rasmi mafunzo hayo. Kushoto ni Bw. Mlay, mkurugenzi rasilimali watu wizara ya utumishi, na kulia ni Bw. Senkondo, mkurugenzi mkuu, TaGLa. Mafunzo haya yanafuatiwa na mafunzo mengine yaliyotolewa kwa maafisa rasilimali watu wa mikoa, wilaya na taasisi zote za UMMA Tanzania.
Dr. Faisal, Katibu Tawala – Kilimanjaro, akisema neon kwa niaba ya washiriki wa mafunzo.

Mafunzo haya yatawaweza maafisa hawa kuufahamu mfumo wenyewe, kujua jinsi mfumo unavyofanya kazi na  kufahamu jinsi ya kutumia taarifa zilizo kwenye mfumo huu ili kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi na kwa haraka.
Washiriki wa mafunzo 
Makatibu Tawala katika picha ya pamoja na mgeni rasmi
Kundi la kwanza la Wakurugenzi katika picha ya pamoja na mgeni rasmi
Kundi la pili la Wakurugenzi katika picha ya pamoja na mgeni rasmi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...