Mgeni Rasmi katika Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,Waziri wa Fedha,Dkt William Mgimwa akitoa hotuba yake wakati akifungua mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha kwa siku tatu mfululizo kuanzia leo Oktoba 2 mpaka Oktoba 5,2013.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF,Dk. Aggrey Mlimuka akitoa hotuba yake mapema leo asubuhi wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF unaofanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,William Erio akizungumza leo kwenye Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa PPF,unaofanyika leo kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,Jijini Arusha.

Kijana Peter William Mulokozi ambaye ni Mwanafunzi wa Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari ya Mzumbe akitoa ushuhuda wake mbele ya Wanachama na Wadau wa PPF waliohudhuria kwenye Mkutano wa 23 wa Mwaka,juu ya PPF ilivyoweza kumsaidia yeye kusoma,mara baada ya Baba yake kupoteza maisha ghafla.PPF ambao ni Mfuko pekee unaotoa fao la Elimu nchini endapo Mwanachama anakuwa amefariki akiwa kwenye ajira.PPF imeweza kumsaidia kijana huyu kusoma mpaka hapo alipofikia.
Kijana Pascalia Nsatto ambaye ni Mwanafunzi wa Kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Kimataifa ya Moshi akitoa ushuhuda wake mbele ya Wanachama na Wadau wa PPF waliohudhuria kwenye Mkutano wa 23 wa Mwaka,juu ya PPF ilivyoweza kumsaidia yeye kusoma,mara baada ya Wazazi wake wote wawili kupoteza maisha.

Ilikuwa ni huzuni tu wakati vijana hao wakitoa ushuhuda wao wa namna walivyoweza kusaidiwa kimasomo na Mfuko wa Pensheni wa PPF pindi walipoondokewa na wazazi wao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...