Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Janet Mbene akishukuru uongozi wa benki ya NMB kwa msaada wa mashuka na vitanda vya akina mama katika hospitali ya Itumba wilaya ya Ileje .Msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni Tano umetolewa na benki ya NMB kupitia tawi la Ileje mwishoni mwa wiki katika viwanja vya hospitali ya Itumba.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ileje, Nd. Mohamed Mwala akimshukuru Meneja wa Kitengo cha Huduma za Serikali wa NMB , Bw. Elieza Msuya baada ya kupokea msaada wa vitanda na mashuka ya hospitali ya wilaya ya vilivyotolewa na benki ya NMB. Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Janet Mbene

Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Janet Mbene akimshukuru Meneja wa Kitengo cha Huduma za Serikali wa NMB , Bw. Elieza Msuya baada ya kupokea msaada wa vitanda na mashuka ya hospitali ya Itumba wilaya ya Ileje vilivyotolewa na benki ya NMB.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...