Familia
ya Kakore ya Dar es Salaam, tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa watu
mbalimbali waliofanikisha shughuli nzima za mazishi ya ndugu yetu mpendwa,
Mwalimu Jasper Rashid Kakore (71), aliyefariki ghafla asubuhi ya Jumapili, Oktoba
20 na kuzikwa Jumatano Oktoba 23 mwaka 2013.
Shukrani
ziwafikie wafanyakazi wote wa Kampuni ya Gapco Tanzania, Kika Contraction, New
Habari 2006 Ltd, Wizara ya Fedha (Hazina) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
(Ukaguzi Kanda ya Mashariki), Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi
ya Pande, Wachungaji, Wainjilisti na watumishi wa K.K.K.T Usharika wa Mramba.
Pia
wanachama wa Umoja wa Wanamtaa wa Tuna wa Dar es Salaam, Wanachama wa Umoja wa
Wanakijiji wa Chome wa Dar es Salaam, Wafanyakazi wote wa Hospitali za Gonja,
Apolo na Hospitali ya Wilaya ya Same, wafanyakazi na wanafunzi wa Shule za
Sekondari Same na Dindimo.
Kadhalika
tunapenda kuwashukuru Wanakijiji wa Gonja na Wanamtaa wa Vuje pia mitandao
mbalimbali ya kijamii (Blogs) ndugu, jamaa na marafiki.
Tunaelewa kuwa watu ni
wengi waliojitoa kwa ajili yetu hivyo kwa yeyote ambaye kwa namna moja ama
nyingine hatukuweza kumtaja tunaomba radhi ila tunathamini sana kile
ulichokitoa kwa ajili yetu.
Kama
familia hatuna la kuwalipa ila Mungu aliyewapa moyo wa kujitoa ndiye atakayewarudishia
mali na kila mlichotoa kwa ajili yetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...