Kwa mara nyingine tena Jumuia ya An Noor ya mjini Leicester nchini Uingereza Iliwakaribisha Waislamu kutoka Leicester na vitongoji mbali mbali kusherehekea Eid el Adh-ha Jumatano ya tarehe 15 Oktoba 2013, Masjid An Noor iliyopo kati kati ya mji iliofurika waumini, wake kwa waume, na kuiachia Kamati Kuu ya Jumuia ya An Noor changamoto ya kutafakari hali itakuwaje Inshaallah pale sherehe nyingine za Eid zitapofanyika mwakani. 
Msikiti ulijaa na kusababisha baadhi ya Waumini kulazimika kuhamia misikiti ya jirani! Pamoja na changamoto hizo, ni dhahiri kulikuwa na mazingira ya kupongezana si tu kwa sababu ya Kusherehekea kukamilika kwa ibada ya Hijja, lakini pia kwa mafanikio ya jamii ya Waislamu kutoka Afrika Mashariki kuweza kufikia malengo yake ya kuwa na kituo cha Kiislamu Kati kati ya mji wa Leicester 
Tafadhali wasiliana nasi kwa maelezo zaidi ya Jumuia hii: 
madrasatulnoor.01@gmail.com 
au Kwa simu: 
Mwenyekiti- Mohammed Omar 44 7903 978481 
Makamu- Abdul Dau 44 779 2104495 
Katibu-Omar Hussein 44 756 5512058



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. kinachonikera hapo ni kufanya hotuba zenu kwa kiingereza wakati tunaojaa hapo ni watanzania.mbona misikiti mingine kama wahindi,wasomali na jamii zingine wanatumia lugha zao.tubadilike tukienzi Kiswahili chetu tuachane na mambo ya woga bila sababu.

    ReplyDelete
  2. Uislamu ni chanzo cha umoja na mshikamano. Unapokereka mdau kwa kiingereza kutumika katika khutba za ijumaa katika msikiti ulioko Uingereza nashindwa kukushangaa.
    Je kama mimi si mswahili unanambiaje?
    Nisije kusali msikitini hapo?
    Nilipohamia uk miaka ya tisini kulikuwa na tatizo hilo, lakini Alhamdulillaah ukiingia misikiti mingi ya waasia sasa lugha inayotumika ni kiingreza.
    Uislamu ni mali ya kila muislamu, si dini ya majimbo.
    Wala si ukabila.
    Mdau Ukerewe

    ReplyDelete
  3. Namwomba Allah ujumbe huu umfikie mdau aliyekerwa na hotuba kufanywa kwa kiingereza wakati majority ni watanzania!
    Ni masikitiko kwamba bado waumini hayajajua hasa nafasi ya msikiti katika jamii ya kiislamu. Mdau anathibitisha hapo juu kuwa kwake yeeye msikiti ni kituo cha ukabila au utaifa.
    Mdau dhana hiyo ni potofu sana na ni hatari kwa jamii ya Waislamu. Msikiti kamwe hauwezi kuchochea utengano baina ya watu. Msomali, mhindi, mwarabu wote mbele ya Allah ni kitu kimoja na inapotokea kuna aina yoyote ya ubaguzi inatakiwa Waislamu wapambane kwa hali zote kuuteketeza.
    An Noor Community ya Leicester imeweka mikakati kuhakikisha kuwa kila aina ya muislamu anakaribishwa Masjid An Noor. Msikiti huu pia una Madrasah ambayo inatumia kiingereza kama lugha ya kufundishia. na hali ni hivyo hivyo inapokuja katika hotuba za Ijumaa, tunajitahidi kufikisha ujumbe kwa umma wa kiislamu. Kwetu kila muislamu ana thamani sawa, na sisi watu wa daawa tuna jukumu la kuwafikishia ujumbe kutoka kwa Allah. Na ndio maana msikiti unaoengeza idadi ya wazungumzaji wa lugha zingine si kuja kusali tu, bali hata kushirikiana nasi.
    Mwenyezi Mungu atuongoze kuuelewa Uislamu kwa mujibu wa mafunzo sahihi, Amin
    Mndengereko, Ukerewe

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...