Katika Gazeti la Mawio Toleo
Namba 0062 la tarehe 26.9.2013 – 02.10.2013 na toleo
Namba 0063 la tarehe 03.10.2013 zimechapishwa habari zenye vichwa vya
habari “Mtandao
wa Ujangili Huu Hapa” na “Wabunge
CCM watajwa ujangili”.
Katika habari zote hizo zimelihusisa
shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kama chanzo cha habari hizo.
Shirika la Hifadhi za Taifa
linapenda kutoa ufafanuzi ufuatao kuhusiana na taarifa hizi:
- Shirika la Hifadhi za Taifa halijawahi kudhamini ripoti iliyotajwa katika habari hizo kuhusiana na utafiti makini wa ujangili.
- Shirika husimamia shughuli za uhifadhi katika maeneo ya Hifadhi
za Taifa pekee kiutendaji, ambapo baadhi ya maeneo
yaliyotajwa
Katika habari hizo kama Selous na Liwale kiutendaji hayapo ndani
ya Shirika la Hifadhi za Taifa.
- Kama Shirika la Umma, hufuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kushirikisha vyombo mbalimbali vya dola katika kushughulikia uhalifu wa aina mbalimbali ikiwemo ujangili.
Ni kwa mantiki hii basi, shirika
linapenda kuweka bayana kuwa halihusiki na taarifa hizo, na hata pale zinapopokelewa zina utaratibu wake
wa kufanyia kazi.
Tunachukua nafasi hii kuviomba
vyombo vya habari kushiriki katika juhudi za kupambana na ujangili kwa kuwa waangalifu katika kuandika
habari za kutuhumiana kabla ya kuwa na ushahidi kamili ambao ni haki
ya kimsingi ya kisheria inayopaswa kuheshimiwa.
Imetolewa na Idara ya Uhusiano
HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA
07/10/2013
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...