Shilole na skwadi lake wakilishambulia jukwaa usiku huu.
pichani juu na chini ni Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria,J-Mrtin akitumbuiza jukwaani usiku wa leo,kwenye tamasha la Serengeti fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,ambaye pia ni mtoto wa Mkongwe wa muziki wa dansi hapa nchini,Mzee Zorro,Maunda Zorro akiimba kwa hisia jukwaani usiku huu kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga wakati tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea.
Mzee wa Masauti,Christian Bella akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu ndani ya uwanja wa Mkwakwani
Sehemu ya mashabiki wakishangweka huku manyunyu ya mvua yakisumbua hapa na pale usiku huu.
Mkali mwingine wa miondoko ya mitindo huru,God Zilla akishusha mistari yake mbele ya mashabiki wake waliokuwa wakiitikia kwa pamoja,ndani ya uwanja wa mkwakwani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea,sambamba na hali ya hewa ya mvua mvua huku mashabiki wakiendelea kupiga mayowe na miluzi kila kona ya uwanja.
Mwanadada Linah ambaye anafanya vyema katika ya muziki wa Bongofleva akicheza na shabiki wake jukwaani.
Msanii ambaye ni muigizaji lakini pia anasumbua sana katika anga ya muziki wa bongofleva,Shilole sambamba na skwadi lake wakilishambulia vilivyo jukwaa usiku huu wakati tamasha la serengeto fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
PICHA ZAIDI INGIA LIVE MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Safi sana

    ReplyDelete
  2. Inaoneka mashabiki wa muziki wa "live" ni madume!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...