Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano a Kimataifa, Mhe. Mahadhi J. Maalim (Mb.) akisikiliza kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na nchi mbalimbali wanachama wa Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano wa Kimataifa kuhusu kuchangia Maendeleo uliofanyika Mjini New York, Marekani tarehe 7 Oktoba, 2013. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy na Bw. Ali Mwadini, Katibu wa Naibu Waziri.




Mhe. Maalim akitoa hotuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania wakati wa Mkutano wa Kimataifa kuhusu Kuchangia Maendeleo (Financing for Development) uliofanyika Mjini New York, Marekani tarehe 7 Oktoba, 2013. Katika hotuba yake Mhe. Maalim alisema kuwa Tanzania inaendelea kupiga hatua katika maendeleo ikiwa ni pamoja na kuongeza jitihada katika ukusanyaji kodi na kuzingatia utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na utawala bora.


Balozi Mushy, Bw. Mwadini pamoja na Bw. Noel Kaganda, Afisa katika Ubalozi wa Tanzania, New York wakifuatilia hotuba hiyo kwa makini.
Kupata hotuba aliyotoa Mhe Mahadhi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...