Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), limeiomba radhi Serikali ya Tanzania kufuatia taarifa waliyoitoa kwenye Mkutano wa 64 wa Kamati Tendaji (EXCOM) ya shirika hilo uliofanyika Geneva, Uswisi tarehe 30 Septemba hadi tarehe 4 Oktoba, 2013. Katika taarifa yao kuhusu Afrika, UNHCR ilieleza kuwa Tanzania imewafukuza Wakimbizi wa Rwanda na Burundi katika operesheni ya kuwaondoa Wahamiaji haramu inayoendelea nchini.
UNHRC imeiomba radhi Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia barua yake ya tarehe 2 Oktoba, 2013. Barua hiyo imeandikwa na Mkurugenzi wa UNHCR Kanda ya Afrika Bw. George Okoth-Obbo (pichani) kwenda kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Pereira Ame Silima  aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo unaofanyika kila mwaka.
Katika barua hiyo, UNHCR imeeleza kusikitishwa na taarifa hiyo ambayo si ya kweli na imekiri kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikishirikiana kwa karibu na UNHRC katika ngazi zote kuhakikisha kwamba hakuna mkimbizi anayerejeshwa kwao katika zoezi la kuwakamata na kuwarejesha kwao wahamiaji haramu linaloendelea nchini Tanzania.
Aidha, Bw. Okoth Obbo ameeleza kuwa UNHCR  na Jumuiya ya Kimataifa kwa ujumla inatambua na kuthamini kwa dhati mchango mkubwa ambao Tanzania imeutoa na inaendelea kuutoa katika kuwahifadhi wakimbizi wa mataifa mbalimbali kwa kipindi cha takribani miaka 40.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea kauli hiyo na kueleza kwamba inatarajia na inaamini kwamba UNHCR itaendelea kutoa taarifa sahihi zenye kutoa picha halisi inayoonesha namna Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyotekeleza wajibu wake  kuwalinda na kuwahifadhi Wakimbizi kwa mujibu wa Sheria za nchi na mikataba ya Kimataifa ambayo nchi imeridhia.
Mwisho.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

06, Oktoba, 2013

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. UNHCR wahakikishe huo waraka wa kuomba radhi wanausambazo duniani kote bila kuwasahau Rwanda, Uganda na Burundi ambao ndio waliwapotosha UNHCR. Hii itasaidia kusafisha jina la nchi yetu mbele ya mataifa mbalimbali na taasis zake.

    ReplyDelete
  2. Naungana na hapo juu. Kuiomba radhi Tanzania peke yake haitoshi. Kama ilivyokwamba taarifa hiyo potofu ilitolewa katika mkutano wa kimataifa, basi ni lazima dunia nzima itaarifiwe kuwa UNHCR walitoa taarifa ya uongo,na kujulishwa ukweli. UNHRC tayari wamechafua jina na nchi yetu. This MUST be a demand from Tanzanian government. Kuiomba radhi Tanzania doesn't remove the bad Picture that UNHCR has imposed on Our lovely Tanzania.

    ReplyDelete
  3. Sielewi kabisa...wanaomba radhi kwani nani aliandika hiyo taharifa...what made them change their mind?

    Haya mashirika hayana tofauti na NGO...uwepo wao unategemea uwepo wa wakimbizi...ndio maana wameamua kwa makusudi ku capitalize kwenye suala la sisi kuwafukuza wahamiaji haramu na ku twist dunia ione ni wakimbizi....

    Na wanaomba msamaha serikali kama ujanja kwa maana kwamba walichoandika tayari kiko noted...watoe press conference tena CNN au media zote zilizotumika kutuchafua. Serikali isikubali hiyo huo msamaha...waiambie dunia kuwa wao ni wahongo...

    Mdau (Mzalendo) The Hague

    ReplyDelete
  4. Kweli wajinga ndio waliwao. Kweli TZ imekubali hivi hivi wakati tayari dunia nzima imesikia hilo na kulaani,

    Nilishangaa Rwanda jeuri waliipata wapi ya kuanziasha chokochoko.

    Huu waraka usambazwe dunia nzima. Tz sio wote mbumbumbu.

    ReplyDelete
  5. Msisahau kuna mtani wetu hapo anaitwa OKOTH.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...