Na Frank Geogrey, Jeshi la Polisi

Mwili wa aliyekuwa Kamanda Mstaafu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kamishina Msaidizi Mwandamizi (SACP) James Kombe utaagwa Ijumaa katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania lililopo Usharika wa Msasani jijini Dar es salaam.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa kamati ya mazishi inayojumuisha Familia ya marehemu na Jeshi la Polisi Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) Thobias Andengenye.

Aliongeza kuwa ndugu, jamaa, marafiki maofisa wa polisi, askari pamoja na viongozi mbalimbali watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu na baadae mwili utasafirishwa kuelekea Moshi, mkoani kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.

James Kombe alifariki dunia Oktoba 22 mwaka huu wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam, Kombe alizaliwa mwaka 1950 huko Mwika mkoani Kilimanjaro na alijiunga na Jeshi la Polisi tarehe 15 mwezi machi mwaka 1970 baada ya kuhitimu elimu ya sekondari mwaka 1969 nchini Uganda ambapo alipandishwa vyeo na kupewa madaraka mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Taifa limepoteza mtumishi wa muhimu sana katika Jeshi la Police.....RIP SACP James Kombe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...