Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiangalia kifaa kipya kabisa cha mawasiliano ya kompyuta Maarufu ipad kwenye kampuni ya Microsoft akishuhudiwa na Waziri wa Biashara Kushoto yake Mh. Nassor Ahmed Mazrui. Kulia yake ni Mtaa lamu wa Kompyuta wa Kampuni ya Maicrosoft Mhandisi Daniel Moloznk na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kati kati akibadilishana mawazo na Mawaziri wake aliofuatanao nao katika ziara yao Nchini Marekani. Kushoto yake ni Mh. Nassor Ahmed Mazrui Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko na kulia yake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed.
Balozi Seif akiagana na Naibu Mkurugenzi wa Mfuko wa Kimataifa wa Misaada wa Bill na Melinda Gates Bibi Arlene Mitchell mara baada yha mazungumzo yao katika Ofisi ya Mfuko huo zilizopo kati kati ya Jiji la Seattle. Kati kati yao ni Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Mh. Nassor Ahmed Mazrui.





Hii ni nafasi nzuri ya kujifunza na kupata maarifa kwa watanzania ila viongozi wetu mpo kibinafsi zaidi na kujitafutia 10% zenu tu.
ReplyDeleteMkirudi huko dili zote mtawapa watoto na ndugu zenu badala ya kulinufaisha taifa letu.
Uncle unaweza kurekebisha hapo maelezo ya picha nathani hiyo computer ambayo mheshimiwa anangalia inaitwa surface tablet ambayo Microsoft wanatengeneza siyo ipad ambayo imetengenezwa na Apple
ReplyDelete