Golikipa wa Mashabiki wa Yanga, Sengerere Yussuf (kushoto), akiluka juu kuokoa mpila ulioelekezwa golini kwake katika Bonanza lililowakutanisha Mashabiki wa Simba na Yanga kupitia Kampeni ya Nani Mtani Jembe inayoendeshwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kweuwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Mkoa wa Morogoro jana.
Beki wa mashabiki wa Yanga, Mussa Said (kushoto) akipambana na mshambilia wa mashabiki wa Simba wakati wa Bonanza liliwakutanisha Mashabiki wa timu mbili hizo kupitia Kampeni ya Nani Mtani Jembe inayoendeshwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Mkoa wa Morogoro jana.
Mashabiki wa Simba na Yanga wakipimana ubavu wa juvuta kamba wakati wa Bonanza ililofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege jana wakati wa kutangaza Kampeni ya Nani Mtani Jembe inayoendeshwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Simba iliwashinda wenza wa yanga.
Shabiki wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Yassin Mwange (kulia), akipuliza Vuvuzela wakati Tamasha la Bonanza lililoandaliwa na Bia hiyo kwaajili ya Mashabiki wa Simba na Yanga Bonanza hilo lilifanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Mkoa wa Morogoro jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...