Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimpa cheti mwanafunzi Nuru Ally aliyefanya vizuri kuliko wanafunzi wote katika somo la Development Studies katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kilichopo mjini Morogoro. Mwanafunzi huyo pia alikabidhiwa zawadi ya Shilingi 50,000. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma SUA, Profesa Peter Gillah. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri karika msomo mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao kesho tarehe 29, Novemba 2013 katika chuo hicho.  Waziri Nchimbi alitoa vyeti na zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni hapo. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Gerald Monela. Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza (CGP) John Minja na Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma, Profesa Peter Gillah
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wapili kushoto aliyevaa tai) wakiwa katika picha ya pamoja na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri karika msomo mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao kesho tarehe 29, Novemba 2013 katika chuo hicho.  Waziri Nchimbi alitoa vyeti na zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni hapo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...