Katibu Mkuu wa CCM Ndugu  Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Lwinga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Namtumbo kwenye uwanja wa Taifa mkoani Ruvuma.Ndugu Kinana na ujumbe wake wapo kwenye ziara ya kikazi mkoani Ruvuma,Mbeya na Njombe katika kukagua Utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama cha CCM,kusikiliza matatizo ya Wananchi  sambamba na kuwahimiza kushiriki katika shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo. Katika Ziara hiyo ya Tunduru na Namtumbo wananchi wamelalamikia kuhusu bei ya zai la Korosho na Tumbaku,kama vile haitoshi wananchi hao walikwenda mbali zaidi kwa kulalamikia suala zima la Mbolea.
 Mbunge wa jimbo la Namtumvo,Vita Kawawa akifafanua jambo kwa Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt.ASharose Migiro pamoja na Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na Uenezi,Nnape Nnauye ndani ya Kata ya Mchomoro Wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.
 Ndugu Kinana na Ujumbe wakielekea kagua ujenzi wa jengo la Wodi ya Wazazi ya akina mama na Watoto kwenye hospitali ya Wilaya ya Namtumbo.
Pichani kulia ni Mbunge wa jimbo la Namtumbo Mh.Vita Kawawa, Katibu wa NEC, Siasa Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye,Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt.ASharose Migiro wakishiriki katika ujenzi wa msingi wa Wodi ya Wazazi na Watoto katika hospitali ya Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.
 Jengo la Utawala wa hospitali hiyo ya wilaya ya Namtumbo.

 Barabara ya kuelekea kwenye hospitali hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM  na Ujumbe wake wakipata taarifa ya mtambo wa kufua umeme katika kituo cha Wilaya ya Namtumbo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...