Mfuko wa pensheni wa LAPF ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii nchini Tanzania wenye makao makuu yake Mjini Dodoma, umekabidhi vifaa vya michezo vyenye thamani ya shilingi milioni tano (5,000,000/=) kwa Chama cha michezo cha Vyuo Vikuu vya Tanzania TUSA, kwa ajili ya mashindano ya TUSA yatakayofanyika mjini Dodoma kuanzia tarehe 10 - 17 Desemba, 2013. Sherehe fupi ya makabidhiano, imefanyika katika Ofisi za LAPF, zilizoko Millennium Towers  jijini Dar es Salaam.
Meneja wa LAPF Kanda ya Dar es Salaa, Bibi Amina Kassim, amesema Mfuko wa Pensheni wa LAPF umekuwa pia ukitoa misaada mbali mbali ya kijamii katika kusaidia sekta mbali mbali kama elimu, hospitali, vituo vya kulea watoto yatima na pia katika sekta ya michezo kusaidia kuinua michezo nchini. 
 Bibi Kassim amesema, hii ni mara ya tatu kwa LAPF kudhamini mashindano kwa mara ya kwanza LAPF ilidhamini mashindano ya mwaka 2011 na 2012, ambapo LAPF imetoa vifaa hivi kwa kutambua umuhimu wa wanafunzi wa taasisis hizo kama wanachama wetu watarajiwa. Amesema kufuatia LAPF kuwa Mfuko bora wa Pensheni kwa kudhihirishwa kwa tuzo iliyotolewa na Msimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii SSRA kuwa LAPF kuwa ni Mfuko wa Pensheni unakua kwa kasi Zaidi nchini. 
Kitendo cha LAPF kuwa imekuwa ikipata tuzo kutoka kwa bodi ya wahasibu nchini NBAA kwa kuwa Mfuko wenye Hesabu Bora za mwaka kwa miaka minne mfululizo kuanzia mwaka 2008, 2009, 2010 na 2011, LAPF sasa imeamua kujikita kudhamini michezi, ili kurudisha kwa jamii, sehemu ya mafanikio hayo. 
 Akishukuru kupata vifaa hivyo, Mwenyekiti wa TUSA Taifa, Asnati Chagu aliishukuru LAPF kwa msaada huo, na kusema umekuja wakati muafaka, ila pia akaomba wafadhili wengine wazidi kujitokeza ili kufanikisha michuona hiyo. 
 Amesema msaada huoiwa jezi ni moja tu ya mahitaji, lakini bado kuna mahitaji mengine yanahitajika vikiwemo vikombe na zawadi kwa washindi mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...