Assalam ´alaykum warahmatullaahi wa Barakatuh
Karibuni nyote katika tovuti yenu:
Tunayo furaha kubwa ya kuwajulisha ndugu zetu Waislamu ya kwamba, kwa hivi sasa tumeafikishwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) kufungua Tovuti maalumu ambayo ni khaswa kwa Wanachuoni tu baada ya maombi ya muda mrefu kutoka kwa baadhi ya ndugu kutokana na uzito waliokuwa wakipata pindi wanapotafuta aitha Fatwa, kitabu au makala; kwani vitu hapo kabla havikuwa sehemu moja na haikuwa sahali kupata kile anachotafuta mtu.
Tovuti yetu tumeonelea kuipa jina la: Wanachuoni.com kutokana na sababu zifuatazo:
1) Hakuna kitachowekwa isipokuwa tu kazi mbalimbali za Wanachuoni - sawa waliotangulia na walioko hivi sasa.
2) Sisi kazi yetu ni kutarjumu (kufasiri) tu zile kazi za Wanachuoni; kama vitabu, makala na fataawa.
3) Usahali wa jina hili, sawa katika kuliandika na kulikumbuka.
Hizi ndizo sababu tatu kuu kuchagua jina hili.
Katika moja ya matunda, natija na faida tunayopata kutoka www.alhidaaya.com mpaka hivi leo, naweza kusema ya kwamba ni pamoja na hivi leo kupatikana Tovuti yenu hii www.wanachuoni.com. Nimesema hayo kutokana na sababu nyingi tu. Hatuna cha kuwalipa wahusika wote wa Alhidaaya zaidi ya kuwaombea Du´aa na kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Azidi kuunufaisha Ummah kupitia tovuti hizi.
Tunachowaomba ndugu zetu ni kuzidi kuwa na subra, kwani tumewaandalia vitu vingi vya Wanachuoni ambao ndio warithi wa Mitume (´alayhimus-Salaam), kukiwemo: vitabu, makala na fatwa ambavyo vimeshakuwa tayari na imebaki kuviweka tu kwenye Tovuti.
Tunaomba msitusahau katika Du´aa zenu za kila siku. Na kila yule mwenye maoni na ushauri juu ya Tovuti yenu hii, tunaomba asikose kutuandikia kupitia kwenye tovuti Wanachuoni kwa juu - kipengele kinachoitwa ”Wasialiana nasi” au kupitia email yetu hii.
Allaah Awajaze kheri nyote.
Ndugu zenu wa:
Wanachuoni.com


.bmp)
Aliyetuummba awaongoze na awape malipo yaliyoyakheri kutokana na yale muyafanyayo kwa ajili Yake tu
ReplyDelete