Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya Kinyago kutoka kwa Makamu wa Mwenyekiti wa CAPA wa Kanda ya Afrika Magharibi, Prof. Daniel Nyarko, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa nne kushoto), Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya CAPA,John Kondoro (kushoto kwa Makamu) na baadhi ya viongozi wa CAPA, wakifurahia kwa pamoja baada ya kuzindua rasmi Jarida la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal), wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. takribani viwanda vyote vya nguo tanzania nadhani hata kenya vinamilikiwa na wahindi, lakini hapa kwenye picha simuoni hata mmoja, je jumuiya hiyo ni ya kina nani haswa? mdau alex bura dar

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...