Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (katikati) akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu matokeo ya utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa.
Afisa Mwandamizi wa Benki ya Dunia Bw. Richard Martini (katikati) akitoa salaam za Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw. Phillipe Dongier, ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kuzingatia vigezo vya tafiti vya kimataifa katika kutoa matokeo ya Mapato na Matumizi ya Kaya nchini.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO,Dar es salaam.
Uwezo wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi nchini kwa mwaka 2011/2012 unaonyesha kuongezeka kutokana na maboresho mbalimbali yaliyofanyika katika sekta ya elimu, afya, umiliki wa biashara, shughuli za kilimo, umiliki wa Vifaa na Rasilimali , makazi bora, ongezeko la shughuli za kiuchumi na ajira.
Akitoa taarifa ya Utafiti ulioendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kuangalia tathmini ya kiwango cha umasikini wa kaya kwa kutumia kipato na masuala mengine yasiyo ya umasikini wa kipato leo jijini Dar es salaam , Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile amesema kuwa kukua kwa kiwango cha elimu, matumizi ya nishati ya umeme, hali ya makazi na umiliki wa rasilimali ni miongoni mwa sababu za kuongezeka kwa uwezo wa mapato na matumizi ya kaya.
Hizi takwimu baada ya hapa zinafanyoiwa nini?
ReplyDelete