Mkongwe wa muziki nchini Congo (DRC) Tabu Ley Rochereau (pichani akiwa amelazwa hospitali) amefariki dunia. Habari zinasema amefariki mapema leo asubuhi huko Ubelgiji alikokuwa amelazwa hospitali akiugua kiharusi.
 Tabuley, aliyezaliwa November 13, 1940, alikuwa kiongozi wa kundi la Orchestre Afrisa International na mmoja wa wasanii wakubwa katika bara la Afrika katika uimbaji na utunzi wa nyimbo. 
Akiwa na mpiga gitaa hodari Dkt Nico Kasanda, Marehemu Tabu Ley alikuwa mwanzilishi wa mtindo wa Soukous, na kuufanya ukubalike kimataifa kwa kuchanganya midundo ya Cuba na Rhumba la Latin Amerika. Tumkumbuke kwa kibao chake "Mokolo Nakokufa"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Mwenyezi Mungu aipmzishe roho yako mahali pema peponi. Ameen

    ReplyDelete
  2. Hii nyimbo sio ya salum Abdallah? Km yake ndiyo nani amekopi na kuppest ?

    ReplyDelete
  3. mokolo nakokufa,siku nitayokufa, alikuwa akivuta hisia na kujiuliza iwapo kifa nchi kavu au majini, jinsi watu watavyolilia, atakumbuka na mikebe ya bia wakinywa mwisho wa mwezi, nk....
    Tumshukuru Mungu kwa Paskali Tabu, tujiulize nasi tutakumbukwa kwa lipi?

    ReplyDelete
  4. R.I.P Tabu Ley

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...