Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo, Imelda Ishuza ( kulia) akipokea cheti ya kuhitimu matunzo toka kwa RC Moro, Joel Bendera.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, ( kulia) akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo Mkuu wa Wilaya ya Makete, Josephine Matiro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( kushoto) akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Norman Sigalla.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera (aliyesimama) akitoa hutuba ya kufunga mafunzo ya Utaalamu wa kilimo cha mazao ya matunda, mboga na mauwa , mjini Morogoro.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Joel Bendera ( wanne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa mafunzo ya utaalamu wa kilimo cha mazao ya ' Horticulture' mjini Morogoro, wakiwemo pia Wakuu wa Wilaya.
Na John Nditi, Morogoro
TAASISI Kilele ya Mazao ya Matunda, Mboga na Maua ‘ Horticulture’( TAHA),imewapatia mafunzo Wakuu wa Wilaya na Wataalamu wa kilimo wa Mikoa ya Kanda ya Kati, Mashariki na Nyanda za Juu kusini juu ya mbinu bora na sahihi za kuboresha na kuendeleza kilimo cha mazao hayo ili kuongeza uzalishaji , kukuza soko la ndani na nje ili kuinua uchumi wa taifa.
Maneja wa Ufundi wa TAHA, Isack Ndamanyere, alisema hayo Novemba 21, mwaka huu mjini hapa , kabla ya kukaribishwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, kufunga mafuzo ya nadharia na vitendo yaliyochukua muda wa tatu ambayo yalindaliwa na Taasisi hiyo na kuwashirikisha washiriki 25.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...