Ofisa uhusino na masoko wa Mpango wa Taifa wa damu salama,Rajab Mwenda (kulia) akielezea kuhusu ripoti ya makusanyo ya damu ya robo mwaka na mikakati ya kukusanya damu kipindi cha Novemba 2013- Januari 2014 wakati wanafunzi wakiwa likizo.
MPANGO wa Taifa wa Damu Salama Tanzania (NBTS) umevuka malengo ya ukusanyaji  damu   kwa asilimia 110  katika kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Septemba 2013 ambapo jumla ya chupa 38,552 zilikusanywa na kuvuka malengo ya chupa 35,000 zilizokuwa zikusanywe.

Ofisa Uhusiano na Masoko wa Mpango wa Damu Salama Tanzania Bw. Rajab Mwenda alisema Kanda iliyongoza kwa makusanyo ya damu ni  Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Dar es Salaam,Morogoro,Dodoma na Pwani  ambako jumla ya chupa 13,669 zilikusanywa, Kanda inayofuatia kwa ukusanyaji damu ni Kanda ya Kaskazini (Kilimanjaro,Arusha, Manyara, Tanga)  iliyokusanya chupa 6,159.

Alisema katika kipindi cha mwezi oktoba 2012 hadi Septemba 2013 takwimu zinaonyesha chupa za damu 139,676 ambayo ni sawa na asilimia 99.8 ya lengo la kukusanya chupa 140,000 ilifikiwa hata hivyo Mpango wa Taifa wa damu salama unakusanya asilimia 26 ya mahitaji ya damu kwa mwaka. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...