Vimbwanga katika ukumbi wa Übersee-Museum mjini Bremen
 Kikosi kazi cha The Ngoma Africa band a.k.a FFU Ughaibuni
Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" a.k.a FFU watarajiwa kutumbuiza usiku wa Jumamosi  Novemba 23, 2013  katika ukumbi wa Übersee-Museum mjini Bremen, nchini Ujerumani.
Wakazi wa jiji la Bremen na miji ya jirani watapata burani ya kung'oa na sululu kutoka kwa mzimu wa muziki Ngoma Africa band ambayo maarufu sana kwa kuwatia kiwewe washabiki wake kila wapandapo jukwaani.
Onyesho hilo limeandaliwa na makumbusho ya Oversee Museum ya jiji la Bremen kwa kushirikiana na Pan African Organization.
Ngoma Africa band wataanza kutumbuiza majira ya saa. 4.00 usiku na kabla ya hapo kutakuwa na maonyesho mbali mbali ya bidhaa za kiafrika,pamoja na vyakula.
Bendi ya "Ngoma Africa " ambayo inadumu kwa muda wa miaka 20 imetajwa kuwa ndio bendi ya mwanzo ya kiafrika kufanikiwa kudumu katika medani ya muziki na kujizolea mamilioni ya washabiki katika kila kona duniani.
Watafiti wa mambo ya muziki wameitaja bendi hiyo kuwa inatumia kila nafasi waliyo nayo kuwanasa washabiki wake,na imetajwa mara nyingi kuwa ni bendi bora na kuchukuwa TUZO za kimataifa, ni bendi ambayo imepachikwa majina mengi mengi ya utani na kiusanii kama a.k.a "FFU Ughaibuni" ,aka "Watoto wa mbwa"  chini ya uongozi wake Kamanda Ras Makunja wa FFU, Mtawala wa
himaya ya  " Anunnaki Empire "

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Watoto wa Mbwa,FFU naona ki-winter kimeshaanza nanyi bado mnaliendeleza gwaride,mbarikiwe amani ya bwana iwe nanyi

    ReplyDelete
  2. kamanda mkuu ras makunja aka fiel-marshal namba 3 afrika,kwanza John Okelo, wa pili Idi Amin Dada na uliobakiwa wewe pekee , Kamanda nauliza hivi ? hamuogopagi baridi ! utauwa vijana baba,msimu wa baridi wewe ndio kwanza unaanza baraha.
    Kila la heri

    ReplyDelete
  3. Baba mtukutu kikamanda ketu ras makunja,mtawala wa himaya ya Anunnaki Elien a.k.a mkuu wa kikosi
    mahususi FFU ughaibuni,baba chonde chonde msimu wa baridi umeanza na wewe ndio kwanza unakaza buti

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...