Tamasha la Filamu za Ulaya mwaka 2013 litaanza rasmi Ijumaa tarehe 22 kwa kuonyesha filamu "Untouchables", kutoka Ufaransa katika ukumbi wa Alliance Française saa mbili kamili usiku.
"Untouchables," filamu iliyofanya vizuri kwa mauzo, iliyotayarishwa mwaka 2011, imewekwa katika mandhari ya Paris na inahusu mabadiliko katika maisha ya msomi kutoka familia inayoheshimika, pindi maisha yake yanapokutana na maisha ya Muafrika, ambaye amemfata ili kumwekea sahihi katika nyaraka yake ya uhifadhi wa jamii (social security) ili aweze kupata mafao yake.
Filamu hii imekuwa ikielezewa kuwa ni filamu iliyochangamka, yenye kutia moyo na yenye mguso katika masuala ya ulemavu na rangi lakini muhimu zaidi, ni filamu kuhusu urafiki.
"Tuna furaha sana kuwaletea filamu hii nzuri katika ufunguzi kwa kupitia Tamasha la Filamu za Ulaya ambayo, ingawa ina muonekano mwepesi, ni filamu inayoangalia hali halisi ya ulemavu na urafiki wa watu wasiolingana," alisema Balozi wa Umoja wa Ulaya Filiberto Ceriani Sebregondi.
Filamu 18 zitaonyeshwa mwaka huu katika kumbi nne, Century Cinemax - Mlimani City , Nafasi Art Space, Goethe - Institut na Alliance Française – zote bila kiingilio.
Waandaaji na waratibu wakiongelea kuhusu tamasha hilo la kila mwaka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...