Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amewaapisha Makamishna
wawili wa Tume ya utumishi wa Mahakama katika hafla fupi iliyofanyika ikulu
jijini Dar es Salaam leo.Walioapishwa katika hafla hiyo ni Dkt.Angelo Mtitu
Mapunda na Mhe.Georgina Mulebya.Pichani Makishna hao Dkt.Angelo Mtitu M apunda
na Mhe.Georgina Mulebya wakila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho
Kikwete(picha na Freddy Maro)
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumatatu, Novemba 6, 2013, amewaapisha Makamishna
wawili wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Tanzania.
Walioapishwa
katika halfa hiyo iliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam ni Dkt. Angelo Mtitu
Mapunda na Ndugu Georgina P.K. Mulebya.
Sherehe
hiyo imehudhuriwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Jaji Mohammed Chande
Othman, Jaji Kiongozi Mheshimiwa Fakhi Jundu, Majaji na watumishi wengine wa
Mahakama.
Imetolewa
na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Novemba, 2013




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...