Sikubahatika
kuonana nawe lakini hadithi zako lukuki nimezisikia,
Kuhusu umahiri wako katika kinanda mpaka ukufunzi wako
mashuleni.
Uongozi wilayani ulishika hatimaye kutinga Bungeni,
Hakika wanaIramba Magharibi
wanakumbuka, sifa zako kwao kamwe hazikomi.
Familia yako uliiongoza, vijana wako wakakua
wasomi,
Kama wewe ulisoma Ulaya, kwanini sisi tuishie
njiani.
Hofu ya Mungu bado tumeishika, mafundisho ya Biblia
hatuwezi acha,
Na mapambio tunazidi imba, tukijikumbusha
kufundisha kwako kwaya.
Kwa kweli Babu ulisifika, kanuni za TANU
ulizishika,
Taifa lako uliitetea, hansard zipo zinatuonyesha,
Uadilifu wako katika kazi tutaendeleza, busara zako
tunazichota,
WanaIramba tutawatetea, kuhakikisha yale yote
mazuri uliyoacha yanaendelea.
Kwa yakini sifa zako kidekede siwezi kumaliza zote,
kwani uhondo uko mwingi,
Lakini hili la mashairi katu siwezi acha, maana
kiburudishayo moyo ni la msingi.
Nabaki tu kujishangaa, haya vipi mjukuu nimeweza
andika,
Hakika uandishi wako mwanana uliwavutia wengi, kama
maji yafatavyo mkondo wake basi urithi wako siwezi kwepa.
Tamati nimefika, sasa yatosha kusema,
Pumzika kwa amani mzee Yona, iko siku isiyo jina
wanaIramba watashuhudia na pasina woga watanena, kwamba wewe kweli ni shujaa wangu
nisiyemuona.
Na Amani
Geoffrey Nkurlu katika kumbukumbu ya 42 ya Hayati Mwalimu Yona Mazeynzile
Nkurlu (Mbunge Iramba Magharibi 1965-1970)
-
06 Novemba 2013



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...