Katibu
Mkuu wa ITU ambalo ni Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia
Mawasiliano Duniani Dr. Hamadoun Toure akisikiliza Maelezo kutoka kwa
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof. John Nkoma. Kulia ni Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. Prof. Makame Mbarawa. Katikati ni
Waziri wa ICT wa Thailand.
Na Innocent Mungy – Bangkok Thailand
Tanzania inashiriki katika Kongano la TEHAMA la Dunia linaloandaliwa
na Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Mawasiliano Duniani
(ITU-International Telecommunications Union) linalofanyika katika jiji
la Bangkok nchini Thailand.
Kongano hilo lenye Kauli Mbiu ya Kuchochea Mabadiliko Katika
Ulimwengu wa TEHAMA, unashirikisha nchi wananchama wa ITU na wasio
wanachama, Makampuni ya Mawasiliano Duniani, Taasisi na wasimamizi wa
sekta ya Mawasiliano Pamoja na Serekali, wanashiriki Kongano hili katika
kipindi ambacho mabadiliko makubwa katika Sekta ya Mawasiliano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...