Kituo cha  Uwekezaji nchini (TIC) kimewashauri wawekezaji wa ndani na nje kutumia fursa inazozitoa  kwa wawekezaji  kuwekeza katika sekta ndogo ya zao  la Korosho ili kuzidi kuongezwa uzalishaji wake.
MkurugenziMtendaji  wa Kituo hicho, Bi. Juliet Kairuki alisema hayo wakati wa mkutano wa wadau wa sekta hiyo kuwa wanahitajika kukitumia kituo chake ili waweze kupata fursa zitakazo wawezesha kuwekeza  zaidi katika uzalishaji zao la korosho.
“Kituo chetu kinahamasisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika sekta hii ambayo ni muhimu sana katika uchumi wa nchi na ustawi wa jamii,” Bi. Kairuki alisema na kuongeza kuwa  kilimo cha korosho ni vyema kipatiwe msukumo zaidi. Alisema kituo kimeweka vivutio mbalimbali kwa wawekezaji ambao wamejidhatiti kuwekeza katika Kilimo, ikiwemo misamaha ya kodi kwa bidhaa za mitaji.
Aliongeza Tanzania bado inahitaji wawekezaji kuwekeza katika Kilimo cha zao hilo, viwanda vya kusindika na kuyatumia masoko ya ndani na nje ya nchi. Hali inaonyesha sekta hiyo haijafanya vya kutosha, hivyo amewaomba  wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kukitumie kituo chake ili kufikia malengo ya serikali katika sekta hiyo.
Sambamba na hilo alisema Tanzania inayomfumo mzuri wa sheria ambayo inavutia kila anayetaka kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo ya Kilimo. Alisema katika mazao ya kilimo, zao la korosho ni la tatu nchini katika kuliingizia taifa mapato hivyo kunakila sababu ya wawekezaji kuingia katika sekta hiyo ndogo.
Pia kuna taasisi za fedha za kutosha kwa ajili ya kupata huduma za kifedha kuendeleza miradi ya Kilimo.Aliongeza kusema soko la hisa linaendelea kukua na imekuwa na msaada mkubwa katika kuhakikisha shughuli za biashara zinazidi kuimarika.
Hata hivyo aliwakumbusha wawekezaji wanaohitaji kuwekeza nchini kuhakikisha wanatii sheria za nchi ili wasiweze kupata misukosuko inayotokana na kuvunja sheria hizo.  Mchumi Mwandamizi Kitengo cha Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bi. Aneth Mathania aliwambia wawekezaji kuwa Tanzania ina ‘barcode’ yake hivyo wakiwekeza mazao yao hayatapata shida ya soko.
“Tanzania imeweka utaratibu mzuri kuhakikisha uzalishaji wa zao hilo katika mnyoro wake wanapata faida, wakiwemo wakulima, wasindikaji na wasafirishaji,”alisema. Pia alisema vifungashia vya zao la korosho vinatolewa na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) hivyo fursa ya uzalishaji zao hilo ni kubwa.
  Mkutano huo uliwaleta wawewkezaji wa ndani na nje wakiwemo ikiwemo  sekta binafsi, taasisi za kifedha, serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na wakulima wadogo kuzungumzia maendeleo ya sekta hiyo ya korosho.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...