MSANII Upendo Nkone amekuwa wa kwanza kuthibitisha kushiriki Tamasha la Krismas litakalofanyika Desemba 25 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema jana kuwa tayari wamefikia makubaliano na msanii huyo na kwamba  bado wanaendelea na mazungumzo na wasanii wengine wa nje na ndani kuhakikisha tamasha hilo la nyimbo za kumsifu mungu linakuwa zuri.
 
“Nafurahi kuwajulisha wapenzi wa muziki wa kiroho kuwa kamati yangu tayari imefikia makubaliano na Nkone, hivyo mambo yatakuwa mazuri kadri siku zinavyokaribia,” alisema Msama.
 
Baadhi ya nyimbo za msanii huyo ni Upendo wa Yesu, Hapa Nilipo, Mungu Baba, Yesu Aliniita, Sikiliza Nikuambie, Usiogope, Ijaposema, Uumbaji, Yesu Nakupenda, Kanisa na Habari Njema.
 
Nyimbo nyingine ni Niacheni Niimbe, Nimebaki na Yesu, Uniongoze Yesu, Nakuhitaji, Acha Uovu, Yesu Atakutunza na Moyo Wangu.Tamasha la Krismas linaandaliwa na Kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es Salaam, ambayo pia huandaa Tamasha la Pasaka kila mwaka.

 Kwa mujibu wa Msama wanataka Tamasha la Krismas liwe bora zaidi kuliko la Pasaka kwa kualika wasanii maarufu kutoka nje na ndani ya Tanzania na kwamba litakuwa tamasha kubwa la nyimbo za kumsifu Mungu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...