Rais  wa  umoja  wa  klabu  za  waandishi  wa habari Tanzania (UTPC) Kenneth Simbaya akimkabidhi  cheti  maalum mmoja kati ya  viongozi wa  vilabu  vya  waandishi  wa habari nchini, vyeti  ambavyo  vinatolewa kwa wanachama wa vilabu ambao  wamepatiwa mafunzo  mbali mbali.




Na  Francis Godwin, Mwanza
UMOJA  wa  klabu  za  waandishi  wa  habari Tanzania (UTPC) umeanza utaratibu wa  kutoa vyeti  maalum kwa  wanachama  wa klabu  za waandishi wa habari nchini  ambao  wanapatiwa mafunzo mbali mbali.

Mkurugenzi  mtendaji  wa  UTPC Abubakar Karsan  alisema  kuwa  vyeti  hivyo vimeanza  kutolewa  baada ya  maadhimio  ya wajumbe  wa mkutano mkuu.
Hivyo  alisema  kuanzia  sasa  wanachama  wa vilabu ambao  watapewa mafunzo wanachama  wake  watapewa vye vyeti maalum .

Pia  alisema  vyeti  hivyo vitakuwa vya  viwango  vya  juu na vinaanza  kutolewa sasa kwa vilabu  hivyo.

Wakati  huo  huo umoja wa  vilabu  vya  waandishi  wa habari Tanzania (UTPC) umewataka  viongozi wa  vilabu  hivyo  mikoani  kutumia changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao kujipanga  badala ya  kuzichukia changamoto hizo.

Kauli  hiyo  imetolewa leo  jijini Mwanza na Rais  wa UTPC Kenneth  Simbaya wakati akifungua mkutano  mkuu  wa  wanachama  wa klabu za  waandishi wa habari.


Simbaya  alisema  kuwa  mbali ya  kuwepo  kwa mafanikio makubwa katika klabu vya waandishi  wa habari nchini ila  bado wapo baadhi ya viongozi ambao wameendelea kukwepa  changamoto  mbali mbali badala ya  kuzifanyia  kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...