Na Edwin Moshi, Makete
Vijana wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kutambua kuwa suala la wao kushiriki mafunzo ya mgambo lipo kisheria hivyo kuitaka jamii kwa ujumla kushirikiana ili malengo ya mafunzo hayo yatimie

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Bi Josephine Matiro wakati akifunga mafunzo ya mgambo yaliyofanyika kwa kipindi cha miezi minne katika kata ya Lupila wilayani Makete

Bi Matiro amefikia hatua hiyo kutokana na risala ya mgambo hao kuonesha kuwa wapo walioandikishwa kushiriki mafunzo hayo lakini waliyakatisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uvivu na kutoona umuhimu wa mafunzo hayo ambapo awali waliandikishwa zaidi ya 150 lakini wamehitimu 61 tu

Katika hatua nyingine Mkuu wa wilaya amewashauri mgambo hao kuanzisha kikundi chao cha ujasiriamali na endapo watafanya hivyo serikali itawapatia mikopo itakayowasaidia kujiendessha kupitia vikundi

Wakizungumza na mtandao huu baadhi ya mgambo waliohitimu kwenye mafunzo wameshukuru na kusema kuwa wameelewa mambo mengi ikiwemo kutumia silaha, kukabiliana na adui hata kama ana silaha, mbinu za kivita pamoja na huduma ya kwanza.
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akikagua gwaride la wanamgambo
 Mkuu wa wilaya akitoa hotuba yake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...