Na Abdulaziz Lindi

Katika heka heka za kuaga mwaka 2013 usiku wa kuamkia leo mji wa Lindi ulitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kushuhudia onyesho la Msanii nyota wa Muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alipokuwa akitoa burudan kabambe katika Tamasha la kudumisha Amani na Maendeleo lililodhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Mtama,Mhe Bernard Membe na kufanyika katika Uwanja wa Ilulu Manispaa ya Lindi na kutoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliodhuria
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’akiwapagawisha mashabikiw wake walikuwa wamefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Ilulu,Mkoani Lindi.
Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’sambamba na madansa wake,wakitoa burudani ya nguvu kwa mashabiki wao.
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambae pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe akipokea salamu toka kwa Diamond alipokuwa akitoa salam za mwaka mpya kwa wana Lindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...