Karibu katika kipindi hiki cha FAMILIA kutoka Jamii Production.
Katika kipindi cha wiki hii, mjadala ulikuwa KWANINI WANANDOA HUTEMBEA NJE YA NDOA?
Mbali na washiriki waliokuwa studio, pia tuliweza kusoma maoni toka kwa wasikilizaji wetu wanaoacha katika kurasa zetu za FACEBOOK
Karibu uungane nasi.
Ukiwa na maoni, maswali ama ushauri usisite kuwasiliana nasi kupitia jamiiproduction@gmail.com
Hamna cha kufanya ee!
ReplyDeleteWangefungua radio za kuwatangazia Wamarekani. Huko Bongo hatuhitaji mawazo yenu. Dunia nzima inajua watu wanaoishi Ughaibuni wana maisha mazuri kuliko nchi zinazoendelea, sasa hakuna sababu ya kudodesha waTz mafanikio yenu huko.
ReplyDeleteKWA NINI WANANDOA HUTEMBEA NJE YA NDOA?
ReplyDeleteJIBU NI MOJA TU NA LINA MATAWI MAWILI (2) TU:
JIBU: ni UJINGA WA MANANDOA
(i)Tamaa:
Wengi huingia ktk ndoa wakiwa na matarajio makubwa zaidi ya uhalisia wa Changamoto halisi zilizopo kwenye Ndoa na Maisha kwa ujumla, hivyo wanapoingia na kukosa walichotarajia ndio hugeukia kwenye (UJINGA WA Tamaa) ya kutembea nje ya Ndoa zao.
(ii)Kuendekeza Umasikini:
Kwa kutokana na sababu Namba (i) juu unakuta miongoni mwa Wanandoa wanakosa uwezo wa Kifikra katika kutafakari jinsi ya kukabiliana na Changamoto za Maisha hivyo wanajikuta ktk (UJINGA WA KUENDEKEZA UMSIKINI) kwa kutembea nje ya Ndoa zao.
Kama Tatizo ni Kipato, pana njia sahihi za kuleta Kipato ktk Ndoa na sio kutoka nje ya Ndoa ama kutafuta chochote ama kubana matumizi.
Mdau wa juu
ReplyDelete...Hamna cha kufanya ee!...
Hilo ni Suala nyeti sana na janga ktk Familia nyingi.
Majumba na Mahusiano ndani yanatetema, yanayumba,
Watu wanalaliana Mzungu wa nne,
Watu wanalaliana na Mapensi ya Jeans!
Harusi nyingi mjini hapa ni feki. Watu wanaiga mapenzi ya kizungu ambayo hayaendani na culture za kiafrika matokeo yake ni talaka ah kwa wengine sio talaka ni kutengana halafu kutafuta mwingine. Hizo sherehe basi ni fahari ambayo wanandoa hawamudu bila ya michango ya lazima. Baadae anaishia kupanga vyumba viwili vya uwani.
ReplyDelete