Marehemu Amina A. Beleko
Leo tarehe 2 Desemba, 2013 umetimiza mwaka mmoja tangu ututoke duniani. Unakumbukwa sana na mimi Mumeo Athumani Beleko, wanao Salim na Adam, Baba na Mama yako, Dada na Kaka zako, Wakwe, Mashemeji na Mawifi zako, Ndugu, Jamaa na Marafiki.
Ni imani yetu kuwa umetutoka kimwili lakini tuko pamoja kiroho. Tutazidi kukuombea dua Mwenyezi Mungu akupumzishe kwa amani Inshallah tutakutana siku ya mwisho.
INNA LILLAH WAINNA ILAYH RAJIUN.
In our hearts you remain. RIP Amina.
ReplyDeleteTunamuombea Allah amsamehe makosa yake na amzidishie mema yake InnshaAllah, Naona hapo hiyo aya narekebisha kidgo ukisema inna lilah sivo unatakiwa umalizie na Inna lilahi wainna ilahi raji'un. hiyo {i} kuwa inamaanisha ni yeye kwake ALLAH, shukran
ReplyDelete"Inna Lillah Wainna Ilayhi Rajiun". Mwenyeez Mungu amughufirie kwa yote na amraham ya arhama r'rahimin. Amlaze pema peponi ndugu yetu marehemu Amina A. Beleko. AMEEN.
ReplyDeleteMdau wa pili umejaribu kukosoa na kusahihisha, lakini na wewe si vibaya ukasahihishwa. Maana aya iloandikwa hapo ipo sahihi "INNA LILLAH WAINNA ILAYH RAJIUN" Ikimaanisha ( HAKIKA YAKE MWENYEEZ MUNGU NA KWA HAKIKA YETU SIE WAJA WAKE BASI KWAKE TUTAREJEA). Sasa ulivyorekebisha na kukosowa wewe, binafsi naona kuna mushkel fulani somewhere.