Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Rais Mstaafu wa Botswana na Mjumbe wa High Level Group Dr. Festus Mogae wakati wa kikao cha Mawaziri wa Elimu na Afya kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika unaofanyika Cape Town nchini Afrika Kusini tarehe 7.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na viongozi waandamizi waliohudhuria mkutano wa High Level Group hukom Cape Town wakisimama kwa dakika moja kwa ajili ya kumkumbuka hayati Rais Nelson Mandela. Kutoka kushoto ni Bwana Enver Surty, Waziri wa Elimu ya Msingi wa Afrika Kusini, Dr. Festus Mogae, Rais Mstaafu wa Botswana, Mama Salma, Bwana Luiz Loures, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, UNAIDS, Dr. Julitha Onabanjo, Naibu Mkurugenzi Mkuu, UNFPA, Bwana Qian Tang, Naibu Mkurugenzi Mkuu-Elimu- UNESCO, Bwana Geeta Rao Gupta, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, UNICEF.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dr. Hussein Mwinyi akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa High Level Group unaofanyika huko Cape Town kuzungumzia elimu ya afya ya uzazi na ukimwi kwa vijana katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipiga picha na Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Bwana Michel Sidibe wakionyesha umuhimu wa dhana nzima ya mkutano wa High Level Group ( YOUNG PEOPLE TODAY, TIME TO ACT NOW) kuhusiana na masuala ya elimu ya afya ya uzazi kwa vjijana katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...