Watu wane wamekufa na wengine 63 kujeruhiwa baada ya Treni ya abiria kuacha reli na kupinduka katika sehemu yenye kona kali maeneo ya Bronx jijini New York, Marekani, mamlaka zimeeeleza.
Gavana Cuomo amesema marehemu watatu wamekutwa nje ya treni na mmoja ndani yake, Hakutaja majina kwa kuwa familia zao bado kujulishwa, na kwamba majeruhi 11 wako mahututi, akiwemo dereva wa treni hilo.
Msemaji wa Metropolitan Transportation Authority, Bi Marjorie Anders amesema sehemu hiyo yenye kona kali iko katika eneo la mwendo mdogo, na kwamba kifaa cha mawasiliano kijulikanacho kama  black box kitafafanua treni hio ilikuwa inasafiri kwa mwendo gani.
Ripota wa Globu ya Jamii aliyekuwa eneo la tukio anafuatilia kujua kama kuna Mtanzania aliyehusika katika ajali hiyo, ikizingatiwa kwamba New York kuna Watanzania wengi wanaoishi jijini humo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...