Mhe. Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa mkutano wa pembezoni uliokuwa umeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Elimu, Sayansi na Utamaduni ( UNESCO) na Baraza la Kimataifa la Sayani ICSU), Balozi Manongi alikuwa kati ya wanajopo wanne walioongoza majadiliano hayo.Wengine kutoka kushoto ni Bi. Vibeke Jense ambaye ni Mkurugenzi wa UNESCO Ofisi ya New York, katikati ni mwedesha majadiliano na kulia kwa Balozi Manongi ni Bw. Gisbert Glaser Mshauri Mwandamizi kutoka Baraza la Kimataifa la Sayansi ( ICSU).
Bw. Hassan Mshinda, ambaye ni Kamishna kutoka Kamisheni ya Sayansi na Teknolojia akichangia katika majadiliano hayo.
sehemu ya washiriki wa mkutano huo.
Washiriki wengine wakifuatili kwa makini majadilianyo hayo kuhusu nafasi ya sayansi na teknolojia katika utekelezaji wa Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu, majadiliano hayo yaliandaliwa kwa ushirikiano wa UNESCO na ICSU.
Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akibadilishana mawazo na Bw. Gisbert Gladser ambaye katika majadiliano hayo, alitaka kufahamu Tanzania inatumiaje uzoefu wake na mafanikio yaliyoainishwa katika majadiliano hayo kuzisaidia nchi nyingine za Afrika akilenga katika uhusiano na ushirikiano baina ya nchi za Kusini ( South- South Cooperation ).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...