Marehemu Mama Laurencia Chande

Familia ya Marehemu Bw & Bibi Boniface Chande wa Mikocheni, Dar es Salaam wanapenda kutoa shukrani zao za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki, majirani na wote walioshiriki nasi katika kipindi chote kigumu cha kumuuguza na hatimae Msiba wa Mama yao mpendwa Laurencia Chande, aliyetwaliwa Tarehe 5/11/2013 na kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele tarehe 8/11/2013 katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Shukrani za pekee ziwaendee wafuatao:-
1.      Dr. Kaduri Mbeni pamoja na wauguzi wote wa TMJ Hospitali
2.      Dr. Robert Moshiro na Dr. Tulizo Shemu wa Muhimbili Hospital
3.      Dr Henry Mwandolela wa Heamieda Clinic Upanga
4.      Mama Cecylia Meshack Gawile wa Mwananyama Hospitali
5.      Chrisant Malege – Muhimbili Hospitali
6.      Fr. Gilbert na Fr. Kasembo wa Parokia ya Mt. Martha Mikocheni kwa huduma za kiroho walizokuwa wakimpatia Marehemu mpaka mauti yalipomfika
7.      Wanachama wa Moyo Mtakatifu wa Yesu wa Parokia ya Mt. Martha Mikocheni kwa sala na maombi.
8.      Wanajumuiya ya Mt. Bernadini Mikocheni
9.      Kikundi cha akina mama wakatoliki (WAWATA) Mikocheni
10.  Jirani Mr. & Mrs. Moshiro
11.  Kikundi cha Akina Mama wa Mikocheni (Mama’s Group)
12.  Kikundi cha Akina Mama wa Charity Women Group
13.  Wafanyakazi wa Benki ya Dunia, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, AAR, na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kwa kutufariji kwa hali na mali katika kipindi chote cha msiba.
14.  Majirani wote kwa ujumla wa Mikocheni, Drive-Inn na TPDC Flats

Kwa kuwa sio rahisi kumshukuru kila mmoja wenu,tunawaomba mpokee shukrani zetu za dhati kabisa kutoka moyoni kwani mmetuonyesha upendo wa hali ya juu na tunawaombea Mungu awabariki sana.

Kutakuwa na Misa ya kumaliza Msiba wa Mama yetu Laurencia Chande itakayofanyika Tarehe 15/12/2013 Parokia ya Mtakatifu Martha Misa ya Saa 1.00 asubuhi na Saa 3.00 Asubuhi na baada ya hapo chakula cha mchana nyumbani kwa Marehemu kuanzia Saa 7 Mchana.

..Nimevipiga vita vilivyo vizuri, imani nimeilinda na mwendo nimeumaliza2 Timoteo 4: 6-8


Bwana alitoa, Bwana ametwaa, 
Jina la Bwana Lihimidiwe. 
AMINA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Poleni sana Faustina, Prisca na familia yote. Mungu awafariji ktk kipindi hiki kigumu.
    Rest in Peace Mama Chande.

    Marina.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...