Mshindi wa kwanza kwa wachezaji wa ridhaa katika mashindano ya gofu ya NSSF,ORYX Tanzania 2013,Frank Roman akikabidhiwa kikombe na katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro Faisal Issa,katikati ni mwakilishi wa wadhamini wa mashindano hayo NSSF,Daudi Mwangole.
Afisa operesheni wa shirika la hifadhi ya jamii NSSF mkoa wa Kilimanjaro Daudi Mwangole akizungumza jambo wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi wa michuano ya Gofu ya NSSF,ORYX Tanzania Open 2013 iliyofanyika katika viwanja vya gofu vya TPC.
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Faisal Issa akimwakilsiha mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama katika utoaji wa zawadi kwa washindi wa michuano ya Gofu ya NSSF,ORYX Tanzania Open 2013 iliyofanyika katika viwanja vya gofu vya TPC.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...