Rais wa Marekani,Barack Obama akihutubia maelfu wa waombolezaji wa Msiba wa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini,Hayati Nelson Mandela waliopo kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg.Rais Obama amemsifia sana Mzee Mandela na kwa mengi aliyoyafanya kwa Waafrika Kusini na Dunia nzima kwa Ujumla.
 Familia ya Hayati Nelson Mandela ikifuatilia misa maalum ya kumuombea kiongozi huyo Maarufu Duniani pamoja na kwamba mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha.
 Maelfu wa wananchi wa Afrika Kusini wakiwa wamefurika kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg
Rais wa Marekani,Barack Obama na Mkewe wakiwa kwenye misa hiyo.
Mke wa zamani wa Hayati Mzee Nelson Mandela, Winnie Madikizela-Mandela akionekana ni mwenye huzuni mkubwa wakati wa ibada maalum iliyofanyika leo kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg.
 Mke wa zamani wa Hayati Mzee Nelson Mandela, Winnie Madikizela-Mandela (kushoto) na mjane wa sasa wa Mzee Mandela,Mama Graca Machel ( kulia mwisho ) wakifuatilia misa hiyo.
 Maelfu wa wananchi walijitokeza katika misa hiyo pamoja na mvua kubwa kunyesha muda mrefu
Wakuu wa nchi mbali mbali Duniani wakiwa kwenye Misa hiyo leo.ambapo Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni mmoja wa viongozi waliopata fursa ya kuhudhuria misa hii.
 Mmoja wa wananchi wa Afrika Kusini akinyoosha mkuno juu kuonyesha ishara ushindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...